Tangaza nasi hapa

Tangaza nasi hapa

JINSI YA KUTATUA (network not available kwenye simu yako) NA KURESTORE SIMU


Hivi ni jinsi ya kurudisha  simu yako ya android kuwa kama ilivotoka kiwandani na KUTATUA tatizo la "network not available". Kitu unachotakiwa kukumbuka katika hili ni kuwa vitu vyote vilivyokuwepo kwenye simu hufutwa na pia inashauriwa kupindi unafanya hivi kuondoa kadi ya simu (Sim Card)lain ya simu pamoja na ‘Memory Card’ au  ‘SD card’. Na kingine ni kuwa hata kama simu ilikuwa na virusi (Virus) basi pia virusi wote hufutwa.
Na hizi ndizo hatua amabazo unaweza kuzifuata ili kufanikiwa ku-restore simu yako. Kwanza hakikisha simu yako imewashwa na kisha fuata hatua zifuatazo:-
  1. Nenda sehemu ilioandikwa ‘Settings'
  2.  Kisha nenda ‘Privancy’ hii ni Kwa baadhi ya smartphone ,aina  nyingine utabonyeza backup and reset alafu factory reset
  3. Utakutana na sehemu ilioandikwa ‘Factory data reset’ kisha gusa factory data reset 
  4.  Utaenda hadi sehemu ilioandikwa ‘Phone reset’ baada ya hapo utapewa onyo ukiulizwa kama kweli una hakika na suala la kufuta kila kitu kwenye simu yako. Ndipo utakubali kwa kwa kugusa ‘Reset phone’ hapo  utasubiri baada ya sekunde kadhaa  simu itaji-restore kama ilivyokuwa mwanzoni.
 Tukumbuke kuwa KURESTORE SIMU kuna saidia hata swala la network Kwa simu za android (smartphone) hivyo ukipata tatizo la "network not available" kwenye simu yako unaweza ukafanya njia hizo hizo pia na tatizo likaisha
Ahsanteni

1 comment:

Powered by Blogger.